Kila mtu anaweza kuhariri makala yoyote, kutoa makosa ya lugha, kutohoa maneno na kuendeleza na kukuza makala, kwa kuandika kwa ufupi au kwa urefu. Tunakushauri ujiandikishe na kufungua akaunti. Angalia Wikipedia:Mwongozo ili ujifunze unavyoweza kuhariri au kusanifisha ukurasa. Usisite kushiriki; kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano, na hautaisha kamwe. Kamusi elezo itaimarika vizuri zaidi kila wakati. Angalia ukurasa wa jumuia, ukurasa wa jamii, na ule wa makala za msingi za kamusi elezo ili kung'amua unaweza kufanya kazi zipi ili kuboresha Wikipedia.
Hamed bin Mohammed el Murjebi (1837 – 14 Juni1905) amejulikana zaidi kwa jina la Tippu Tip. Alikuwa mfanyabiashara mashuhuri katika Afrika ya Mashariki na Kati wakati wa karne ya 19.
Babake alikuwa mfanyabiashara Mwarabu Muhammed bin Juma, mamake aliitwa Nyaso. Hamed aliingia katika shughuli za biashara tangu umri wa miaka 12 akafaulu katika biashara ya misafara kati ya Zanzibar na Kongo. Alipanga misafara ya mahamali waelfu akipeleka bidhaa kutoka Bagamoyo kupitia Tabora hadi Ujiji kwa Ziwa Tanganyika na ndani ya Kongo. Bidhaa alizobeba alitumia kujipatia pembe za ndovu na watumwa; watumwa walisaidia kubeba pembe za ndovu njia ya kurudi hadi pwani. Hemed alitajirika sana. Athira yake ilipanuka katika Kongo ya Mashariki hadi alitawala eneo kubwa sana.
TANGAZO LA KIFO cha Ingo Koll au Kipala kilichotokea tarehe 10, Julai, 2023 nchini Ujerumani. Kipala alikuwa mchangiaji mashuhuri wa Wikipedia kuanzia Disemba 2005 hadi Juni 28, 2023. Siku kumi na mbili mbele tangu kuhariri Wikipedia yetu kwa mara ya mwisho, Mola Jalali Muumba wa mbingu na ardhi, alitwaa kiumbe chake. Kipala atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa wa kuhariri Wikipedia hii. Kwanza akiwa kama msimamizi (admin) baadaye mrasimu (bureaucrat) ambaye ametoa haki za usimamizi kwa wakabidhi ama wasimamizi wengine kama Muddyb, Antoni na wengine wengi tu. Miaka kumi na nane ya kusimamia na kutunga makala mbalimbali itakumbukwa hadi mwisho wa dunia ya Wikipedia. Kipala amechangia makala za aina mbalimbali ikiwemo, muziki, filamu, tiba, elimu ya nyota, dini, siasa, demografia, jiografia, sayansi, na mengine mengi. Amepata kuwa msaada mkubwa kwa wachangiaji wapya kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Alianzisha Jenga Wikipedia ya Kiswahili kwa lengo la kuboresha makala mbalimbali na kutoa mafunzo kwa watu wapya. Pengo lake halitazibika. Sisi wanajumuia ya Wikipedia ya Kiswahili tunasikitika kutangaza kifo chake!
Takwimu ya Wikipedia ya Kiswahili
Idadi ya makala: 81,932
Idadi ya kurasa zote: 176,222 (pamoja na kurasa za watumiaji, majadiliano, msaada n.k.)
Katika mwezi wa Agosti 2020 wikipedia ya Kiswahili iliangaliwa mara milioni 1.73 hivi, ambayo ni sawa na mara 55,800 kwa siku au mara 2,326 kila saa. Asilimia 52 za wasomaji wetu wako Tanzania, asilimia 13 wako Kenya, asilimia 18 wako Marekani na mnamo asilimia 10 wako Ulaya.
(fungua anwani kwa browser yako, ondoa majina yaliyopo na ingiza jina la makala (hadi makala 10) unayopenda. Unaweza kubadilisha kipindi cha taarifa utakachoona; takwimu kabla ya 2015 hapa)
na makala 100 zilizotazamiwa zaidi "Topviews" kwa kipindi fulani.
(unachagua kati ya makala 100 kwa mwezi au kwa siku)
Kamusi elezo ya Wiki ni kamusi elezo huru iliyo chini ya Shirika Lisilo la Kiserikali la Wikimedia Foundation, ambalo linasimamia miradi mingine mbalimbali ambayo imeorodheshwa hapo chini. Mpaka sasa miradi inayopatikana Kiswahili ni Wikipedia na Wikamusi. Wikitabu imewekwa Kiswahili lakini bado ni tupu. Mengine inapatikana Kiingereza pamoja na lugha tofauti.