Yemen

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
الجمهورية اليمنية
Al-Jumhūriyyah al-Yamaniyyah

Jamhuri ya Yemen
Bendera ya Yemen Nembo ya Yemen
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Allah, al-Watan, at-Thawra, al-Wehda
(Mungu, taifa, mapinduzi, umoja)
Wimbo wa taifa: Jamhuri ya Maungano
Lokeshen ya Yemen
Mji mkuu Sana'a
15°21′ N 12°24′ E
Mji mkubwa nchini Sana'a
Lugha rasmi Kiarabu
Serikali Jamhuri
Abd Rabbuh Mansur Hadi
Khaled Bahah
Establishment
Maungano ya Yemen Kaskazini
na Kusini

22 Mei 1990
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
528,076 km² (50)
kidogo sana
Idadi ya watu
 - Julai 2013 kadirio
 - 2004 sensa
 - Msongamano wa watu
 
25,408,000 (48)
19,685,000
44.7/km² (160)
Fedha Yemeni rial $1 = 198.13 Rials (YER)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+3)
(UTC)
Intaneti TLD .ye
Kodi ya simu +967

-



Yemen (Kiarabu: الجمهورية اليمنية ) ni nchi kusini mwa Bara Arabu.

Imepakana na Omani, Saudia na Bahari Hindi.

Nchi za karibu ng'ambo ya mlango wa bahari wa Bab el Mandeb ni Eritrea, Jibuti na Somalia.

Eneo lake ni pamoja na kisiwa cha Sokotra na visiwa 200 vingine.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Hadi mwaka 1990 palikuwa na nchi mbili za Yemen ya Kaskazini na Yemen ya Kusini zilizoungana tarehe 22 Mei 1990.

Ile ya kaskazini ilikuwa Ufalme wa Yemen baada ya Imamu Yahya Muhamad wa kundi la Zaidiya kuvamia velayat ya Yemen ya milki ya Waturuki Waosmani (1 Novemba 1918). Baadaye ikawa Jamhuri kwa njia ya mapinduzi (1962).

Ile ya kusini ilikuwa sehemu koloni (Aden) na sehemu nchi lindwa (Hadramaut) ya Waingereza. Baada ya ukoloni kwisha ikawa mara moja Jamhuri (30 Novemba 1967).

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wengi ni Waarabu wa makabila mbalimbali; wengine ni machotara wa Kiarabu-Kiafrika, Waajemi na Wazungu.

Lugha rasmi na ya kawaida ni Kiarabu.

Upande wa dini, wananchi karibu wote (99%) ni Waislamu, wakiwemo Wasuni (60–65%) na Washia (35-40%). Waliobaki ni Wakristo, Wayahudi, Wahindu au hawana dini yote.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Japan | Kambodia | Kazakhstan | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Kirgizstan | Laos | Lebanon | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Urusi1 | Saudia | Singapore | Sri Lanka | Syria | Taiwan (Jamhuri ya China) | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Ufilipino | Uthai | Uturuki1 | Turkmenistan | Uhindi | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi hii iko Asia lakini kwa sababu za kihistoria au kiutamaduni inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya. 3. Eneo la pekee la China.


Flag of Yemen.svg Makala hii kuhusu maeneo ya Yemen bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Yemen kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.