Kila mtu anaweza kuhariri makala yoyote, kutoa makosa ya lugha, kutohoa maneno na kuendeleza na kukuza makala, kwa kuandika kwa ufupi au kwa urefu. Tunakushauri ujiandikishe na kufungua akaunti. Angalia Msaada wa kuanzisha makala ili ujifunze unavyoweza kuhariri au kusanifisha ukurasa. Usisite kushiriki; kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano, na hautaisha kamwe. Kamusi elezo itaimarika vizuri zaidi kila wakati. Angalia ukurasa wa jumuia, ukurasa wa jamii, na ule wa makala za msingi za kamusi elezo ili kung'amua unaweza kufanya kazi zipi ili kuboresha Wikipedia.
Je, wajua...
Kutoka kwenye mkusanyiko wa makala za Wikipedia:
... kwamba Ngorongoro imepokelewa katika orodha ya urithi wa dunia ya UNESCO?
Ulemavu ni hali ya kuwa na hitilafu ya kudumu mwilini au akilini inayomzuia mtu kutekeleza shughuli zilizo kawaida katika maisha ya jamii. Unamwekea mtu mipaka asiweze kutekeleza shughuli fulani katika maisha yake, tofauti na watu wengine.
Hitilafu na ulemavu
Shirika la Afya Duniani (WHO) limeunda mfumo wa kupanga alama za ulemavu. Hapa kuna tofauti kati ya
hitilafu (ing. impairment) kama kukosa uwezo wa kutumia kiungo cha mwili kama kawaida
ulemavu (ing. disability) kama hitilafu inasababisha kukosa uwezo wa kutekeleza shughuli zinazotekelezwa na "watu wa kawaida".
hasara au kikwazo (ing. handicap) inayoweza kupatikana kwa mtu mwenye ulemavu akishindwa kutekeleza shughuli katika jamii.
Kwa mfano mtoto aliyeambukizwa ugonjwa wa kupooza (ing. cerebral palsy) anabaki na hitilafu ya viungo vya miguu hawezi kuvikunja wala haiwezi kubeba uzito wa mwili wake. Hitilafu hii inamzuia kutembea kwa njia ya kawaida. Kama hatibiwi hitilafu inaweza kuongezeka kwa sababu musuli ya miguu zinajikaza zaidi na zaidi. Kukosa uwezo wa kutembea ni ulemavu. Lakini kiwango chake kinaweza kupunguzwa kwa tiba na vifaa vya pekee. Akijifunza kutembea kwa kutumia vyuma vilivyofungwa kando la miguu vizuizi vya kutekeleza shughuli vinapungua sana. Kutegemeana na mazingira anapoishi ataona hasara ndogo au kubwa zaidi akitafuta njia yake katika maisha. ►Soma zaidi
Picha nzuri ya wiki
Ng'ombe ni wanyama wakubwa wa jenasi Bos. Spishi ya ng'ombe ina nususpishi au aina nyingi lakini ni spishi moja tu.
Ng'ombe hula manyasi na kutembea kwa vidole viwili. Asili yake ni aina za ng'ombe wa pori waliofugwa kwa sababu ya nyama na maziwa. Katika nchi nyingi anatumiwa pia kama mnyama wa mizigo anayevuta plau au magari.
Wataalamu huamini ya kwamba aina zote za ng'ombe zina asili katika mashariki ya kati mnamo milenia ya 9 KK ambako watu waliwahi kuwafuga nas kutoka hapa ufugaji ng'ombe ulisambaa kote duniani.
Takwimu ya Wikipedia ya Kiswahili
Idadi ya makala: 30,527
Idadi ya kurasa zote: 75,753 (pamoja na kurasa za watumiaji, majadiliano, msaada n.k.)
(baada ya kufungua anwani kwa browser yako, badilisha "Mwanzo" kwa jina la makala husika, na badilisha namba 2 za mwisho -sasa "10" kwa Oktoba- kwa mwezi unaopenda kuona au namba 4 za kwanza kwa mwaka)
Jumuia za Wikimedia
Kamusi elezo ya Wiki ni kamusi elezo huru iliyo chini ya Shirika Lisilo la Kiserikali la Wikimedia Foundation, ambalo linasimamia miradi mingine mbalimbali ambayo imeorodheshwa hapo chini. Mpaka sasa miradi inayopatikana Kiswahili ni Wikipedia na Wikamusi. Wikitabu imewekwa Kiswahili lakini bado ni tupu. Mengine inapatikana Kiingereza pamoja na lugha tofauti.