Tunda

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Fyulisi kama mfano wa tunda:
katikati iko kokwa yenye mbegu;
sehemu nene la nyama ya tunda ambayo ni sehemu ya kuliwa
ganda la nje kabisa linafunika tunda lote kama ngozi.
Sahani ya matunda

Matunda ni sehemu ya mimea kama miti au vichaka vyenye mbegu ndani yake.

Kwa lugha ya biolojia ni ovari ya ua iliyoiva na kuwa na mbegu ndani yake.

Kwa lugha ya kila siku ni zaidi sehemu hiyohiyo kama ina pande zinazoliwa.

Ua la mmea kama imeendelea kukuza mbegu hufunika mbegu mwenyewe kwa ganda la kuukinga. Ganda hili mara nyingi lina sehemu ya nyama ya tunda. Kama sehemu hii ina lishe kwa mwanadamu na ladha ya kupendeza basi ni tunda la kuliwa.

Matunda mengi yana maji ndani yake pamoja na sukari asilia. Asilimia kubwa ya tunda ni nyuzi ya kitembwe. Ina kiasi kikubwa cha vitamini na madini kama chuma. Kwa kawaida matunda hayana proteini na mafuta mengi isipokuwa matunda ya pekee.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Morpho didius Male Dos MHNT.jpg Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tunda kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.